top of page
ufafanuzi_banner_2.jpg

Karibuni wote kwenye tovuti ya Kanisa la Biblia Publishers

Hongera kwa nia yako ya kusoma Neno la Mungu. Tunategemea tunaweza kukusaidia kwa njia mbalimbali ili ulielewe na kulitangaza Neno la Bwana na kueleza ujumbe wa Yesu Kristo kwa watu walio karibu na walio mbali. Chunguza tovuti hii vizuri ili ujipatie vitabu vinavyofaa kwa maisha na huduma yako. Vitabu vyetu vinapatikana katika maduka mbalimbali ya Kikristo katika nchi ya Tanzania. 

MPYA

Ufafanuzi Hai wa Biblia (Believer‘s Bible Commentary) ni kitabu kinachotoa maelezo ya kila mstari wa Biblia kwa upana na kwa kina sana. Katika nyaraka zake Mtume Paulo, anahimiza maisha ya kushirikiana vema katika familia, katika Kanisa na katika jamii. Pia analieleza Kanisa limwone Yesu Kristo ili lijiandae kwa kurudi kwake.

KAZI YETU

Kazi yetu ni kutafsiri, kuandaa na kutoa maelezo ya Biblia kwa Kiswahili. Lengo letu ni kutoa vitabu ili watu wapate kufahamu Biblia vizuri zaidi, wakiishaelewa wenyewe wawafundishe wengine Neno la Mungu na kutafsiri maana yake kwa maisha ya kila siku. 

9H8A4572.jpg
emmaus_mchungaji.jpg

EMMAUS SCHULE YA BIBLIA KWA YA POSTA

inahudumia watu wote wanaopenda kusoma Biblia kwa njia ya posta. Masomo na mitihani yanatumwa kwa mwanafunzi. Baada ya kujaza anarudisha mtihani na malipo kwenye ofisi zetu. 

Tuma maulizo kwa SMS, Simu au whatsapp +255 765 442 452

Email: emmaus.dodoma@kanisa-la-biblia.org

 

Inawezekana kusoma Emmaus kwa njia ya mtandao. Pakua Emmaus-App kwenye simu kwa kutumia playstore. Kusoma kwenye mtandao ni bure.

 

Jina la Emmaus linatokana na jina la kijiji kimoja katika Biblia ambako wanafunzi wawili walikuwa wanaelekea walipotokewa na Bwana Yesu baada ya kufufuka kwake, na alipokuwa anawaelezea maandiko, Luka 24:13.

UKITAKA KUPATA MAELEZO ZAIDI

Hapa unaweza kuagiza orodha yetu ya bei za vitabu.

Asante kwa kuandika.

KLB PUBLISHERS ON SOCIAL MEDIA

  • Instagram
bottom of page